Habari mbalimbali ambazo zinazidi kusambaa mtandaoni na pia katika vyombo mbalimbali vya habari vikiwemo vile vya kimataifa kama vile CNN, The Guardian UK,Reuters,AFP,Al Jazeera nk zinasema kwamba aliyekuwa Rais wa Libya,Moammar Ghadhafi, amefariki dunia baada ya kushambuliwa na kuumizwa vibaya katika mapambano makali yaliyotokea katika mji aliozaliwa wa Sirte kati ya waasi(National Transitional Council-NTC) na majeshi yake.
Kwa mujibu wa msemaji wa NTC,Abdel Majid Mlegta,Ghadhafi ambaye aliitawala Libya kwa miaka takribani 42, amefariki kutokana na kuumizwa vibaya kichwani wakati wa mashambulizi hayo na wakati akijaribu kukimbia.
Hizi hapa ni baadhi ya picha ambazo zinazidi kusambaa mtandaoni zinazoonyesha sura ya Moammar Ghadhafi baada ya mashambulizi.Tunaomba radhi kwa picha hizi!
0 comments:
Post a Comment