Tuesday, December 27, 2011
Black Rhino au Black Chata,bila shaka bado walikumbuka na kulitambua jina hilo.Nimeanza kwa kusema kwamba bila shaka walikumbuka kwa sababu kwa muda kiasi Black Rhino au jina halisi Nicholaus Haule alikuwa kimya kidogo katika masuala ya muziki.Mwenyewe anasema maisha ilibidi ayaelekezee kwingine kidogo.Akaenda chuoni na kupata wakti wa kuvaa lile joho(la shule ya wakubwa na sio chekechea) na kisha baada ya hapo akaanza “mzigo” kama watu wengine. Kukaa kwake kimya kukatafsiriwa na watu wengine kwamba ndio amekacha muziki au muziki umemkacha.Hapana! He is back and doing what he knows best;good music. Na mara hii,pamoja na elimu aliyonayo,bila shaka hata soko la muziki atakuwa analiangalia tofauti. Juu ya yote,Black Rhino anathibitisha kwamba ukitoka kwenye familia ya muziki,basi muziki kamwe haukuachi na wewe huna jinsi bali kwenda nao sambasamba.Majina mengine kutoka katika familia yake ni kama vile The Heavy Weight MC,Professor Jay,Kolihombi,Simple X na Mr.Teacher.

 Wimbo unaitwa Taking Ova.Umetengenezwa pale Dhahabu Records chini ya Producer anayekuja juu sana anayekwenda kwa jina Mbezi.Sikiliza Taking Ova hapa chini;

0 comments:

LinkWithin

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

CONTACT US

Lukata Willy,
BK,
Houston TX,
U.S.A

Tel:
832-859-6047
E-Mail:
lukatawilly@ymail.com
http://angrybirdsgamer.com

Total Pageviews

NEW EAST AFRICA SONG



Lukata Willy

Lukata Willy
ITS NOT WHAT YOU HAVE IN YOUR LIVE, BUT WHO YOU HAVE IN YOUR LIFE THAT COUNTS

FOLLOWER US ON

BONGOFLAVA

Like Us on Facebook

COUNTRY VISIT MY WEB

Home

Create by Bongotrack. Powered by Blogger.

BLOG FANS